Psalms 126:1-3

Kurejezwa Kutoka Utumwani

(Wimbo Wa Kwenda Juu)


1 a Bwana alipowarejeza mateka Sayuni,
tulikuwa kama watu walioota ndoto.

2 bVinywa vyetu vilijaa kicheko,
ndimi zetu zilijaa nyimbo za shangwe.
Ndipo iliposemwa miongoni mwa mataifa,
Bwana amewatendea mambo makuu.”

3 c Bwana ametutendea mambo makuu,
nasi tumejaa furaha.

Copyright information for SwhKC